Zaburi 1

Zaburi 1

KITABU CHA KWANZA

Furaha ya kweli

1Heri mtu asiyefuata shauri la waovu,

asiyeshiriki njia za wenye dhambi,

wala kujumuika na wenye dharau;

2bali huifurahia sheria ya Mwenyezi-Mungu,

na kuitafakari mchana na usiku.

3Huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito,

unaozaa matunda kwa wakati wake,

na majani yake hayanyauki.

Kila afanyalo hufanikiwa.

4Lakini waovu sivyo walivyo;

wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.

5Kwa hiyo watu waovu wataanguka wakati wa hukumu,

wenye dhambi hawatakaa na kusanyiko la waadilifu.

6Maana Mwenyezi-Mungu huziongoza njia za waadilifu;

lakini njia za waovu zitaishia katika maangamizi.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania