The chat will start when you send the first message.
1Mshangilieni Mwenyezi-Mungu, enyi nchi zote!
2Mwabuduni Mwenyezi-Mungu kwa furaha,
nendeni kwake mkiimba kwa shangwe!
3Jueni kwamba Mwenyezi-Mungu ni Mungu.
Yeye ndiye aliyetuumba, nasi ni mali yake;
sisi ni watu wake, ni kondoo wa malisho yake.
4Pitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani,
ingieni katika nyua zake kwa sifa.
Mshukuruni na kulisifu jina lake.
5Mwenyezi-Mungu ni mwema;[#Taz Zab 106:1; 107:1; 136:1]
fadhili zake zadumu milele,
na uaminifu wake katika vizazi vyote.