Zaburi 93

Zaburi 93

Mungu mfalme

1Mwenyezi-Mungu anatawala;

amejivika fahari kuu!

Mwenyezi-Mungu amevaa fahari na nguvu!

Ameuimarisha ulimwengu, nao hautatikisika kamwe.

2Kiti chako cha enzi ni imara tangu kale;

wewe umekuwapo kabla ya nyakati zote.

3Vilindi vimetoa sauti, ee Mwenyezi-Mungu;

naam, vimepaza sauti yake,

vilindi vyapaza tena mvumo wake.

4Mwenyezi-Mungu ana enzi kuu juu mbinguni,

ana nguvu kuliko mlio wa bahari,

ana nguvu kuliko mawimbi ya maji.

5Ee Mwenyezi-Mungu, maagizo yako ni thabiti;

nyumba yako ni takatifu milele na milele.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania