Zaburi 54

Zaburi 54

Sala ya kujikinga na maadui

1Uniokoe, ee Mungu, kwa jina lako;

unitetee kwa nguvu yako.

2Uisikie, ee Mungu, sala yangu;

uyategee sikio maneno ya kinywa changu.

3Watu wenye kiburi wananishambulia;

wakatili wanayawinda maisha yangu,

watu ambao hawamjali Mungu.

4Najua Mungu ni msaada wangu,

Mwenyezi-Mungu hutegemeza maisha yangu.

5Yeye atawaadhibu maadui zangu kwa uovu wao wenyewe;

kwa uaminifu wako, ee Mungu, uwaangamize.

6Nitakutolea tambiko kwa moyo mkunjufu;

nitakushukuru kwa kuwa ni vema.

7Maana umeniokoa katika taabu zangu zote,

nami nimewaona maadui zangu wameshindwa.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania