Zaburi 136

Zaburi 136

Zaburi 136

Wimbo wa kumshukuru Mwenyezi Mungu

1Mshukuruni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ni mwema.

2Mshukuruni Mungu wa miungu.

3Mshukuruni Bwana wa mabwana:

4Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu,

5Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu,

6Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji,

7Ambaye aliumba mianga mikubwa,

8Jua litawale mchana,

9Mwezi na nyota vitawale usiku,

10Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri,

11Na kuwatoa Israeli katikati yao,

12Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa,

13Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu,

14Na kuwapitisha Israeli katikati yake,

15Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu,

16Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa,

17Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu,

18Naye aliwaua wafalme wenye nguvu,

19Sihoni mfalme wa Waamori,

20Ogu mfalme wa Bashani,

21Akatoa nchi yao kuwa urithi,

22Urithi kwa Israeli mtumishi wake,

23Aliyetukumbuka katika unyonge wetu,

24Alituweka huru toka adui zetu,

25Ambaye humpa chakula kila kiumbe.

26Mshukuruni Mungu wa mbinguni,

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.