Zaburi 138

Zaburi 138

Zaburi 138

Maombi ya shukrani

1Nitakusifu wewe, Ee Mwenyezi Mungu, kwa moyo wangu wote,

mbele ya “miungu” nitaimba sifa zako.

2Nitasujudu nikielekea Hekalu lako takatifu,

nami nitalisifu jina lako

kwa ajili ya upendo wako

na uaminifu,

kwa maana umeitukuza ahadi yako

zaidi ya jina lako.

3Nilipoita, ulinijibu;

ulinifanya jasiri na mwenye moyo hodari.

4Wafalme wote wa dunia wakusifu wewe Ee Mwenyezi Mungu,

wakati wanaposikia maneno ya kinywa chako.

5Wao na waimbe kuhusu njia za Mwenyezi Mungu,

kwa maana utukufu wa Mwenyezi Mungu ni mkuu.

6Ingawa Mwenyezi Mungu yuko juu,

humwangalia mnyonge,

bali mwenye kiburi

yeye anamjua kutokea mbali.

7Nijapopita katikati ya shida,

wewe unayahifadhi maisha yangu,

unanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu,

kwa mkono wako wa kuume unaniokoa.

8Mwenyezi Mungu atatimiza kusudi lake kwangu,

Ee Mwenyezi Mungu, upendo wako wadumu milele:

usiziache kazi za mikono yako.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.