Zaburi 43

Zaburi 43

Zaburi 43

Maombi ya mtu aliye uhamishoni yanaendelea

1Ee Mungu unihukumu,

nitetee dhidi ya taifa lisilomcha Mungu,

niokoe na watu wadanganyifu na waovu.

2Wewe ni Mungu ngome yangu.

Kwa nini umenikataa?

Kwa nini niendelee kuomboleza,

nikidhulumiwa na adui?

3Tuma hima nuru yako na kweli yako viniongoze;

na vinilete hadi mlima wako mtakatifu,

mahali unapoishi.

4Ndipo nitaenda madhabahuni pa Mungu,

kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu.

Nitakusifu kwa kinubi,

Ee Mungu, Mungu wangu.

5Ee nafsi yangu, kwa nini unasononeka?

Kwa nini unafadhaika hivyo ndani yangu?

Weka tumaini lako kwa Mungu,

kwa sababu bado nitamsifu

Mwokozi wangu na Mungu wangu.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.