Zaburi 96

Zaburi 96

Zaburi 96

Mungu Mfalme mkuu

(1Nya 16:23‑33)

1Mwimbieni Bwana wimbo mpya;

mwimbieni Bwana dunia yote.

2Mwimbieni Bwana , lisifuni jina lake;

tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

3Tangazeni utukufu wake katika mataifa,

matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.

4Kwa kuwa Bwana ni mkuu mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote;

yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.

5Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu,

lakini Bwana aliziumba mbingu.

6Fahari na enzi viko mbele yake;

nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.

7Mpeni Bwana , enyi jamaa za mataifa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu.

8Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;

leteni sadaka na mje katika nyua zake.

9Mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake;

dunia yote na itetemeke mbele zake.

10Semeni katika mataifa kwamba, “Bwana anatawala.”

Ulimwengu ameuweka imara, hauwezi kusogezwa;

atawahukumu watu kwa uadilifu.

11Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi;

bahari na ivume, na vyote vilivyo ndani yake;

12mashamba na yashangilie,

pamoja na vyote vilivyomo.

Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;

13itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja,

anakuja kuihukumu dunia.

Ataihukumu dunia kwa haki,

na mataifa katika kweli yake.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.