Zaburi 99

Zaburi 99

Zaburi 99

Mungu Mfalme mtakatifu

1Bwana anatawala,

mataifa na yatetemeke;

anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

2Bwana ni mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

3Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

4Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

5Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

6Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita Bwana ,

naye aliwajibu.

7Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

8Ee Bwana , wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.