The chat will start when you send the first message.
1Hayo yalipokwisha, Dawidi akawapiga Wafilisti, akawashinda, akauchukua Gati na vijiji vyake mikononi mwa Wafilisti.
2Akawapiga nao Wamoabu, hao Wamoabu wakawa watumishi wa Dawidi, wakamletea mahongo.
3Kisha Dawidi akampiga Hadarezeri, mfalme wa Soba ulioko upande wa Hamati, alipokwenda kuusimika tena ufalme wake huko kwenye jito la Furati.
4Dawidi akateka kwake magari 1000, na wapanda farasi 7000 na askari waliokwenda kwa miguu 20000, nao farasi wote wa kuvuta magari Dawidi akawakata mishipa ya miguu, akajisazia farasi wa magari mia tu.
5Washami wa Damasko walipokuja kumsaidia Hadarezeri, mfalme wa Soba, Dawidi akapiga kwao Washami watu 22000.
6Dawidi akaweka askari kwao Washami wa Damasko, hao Washami wakawa watumishi wa Dawidi, wakamletea mahongo. Ndivyo, Bwana alivyompa Dawidi kushinda pote, alipokwenda.
7Dawidi akazichukua ngao za dhahabu, watumishi wa Hadarezeri walizokuwa nazo, akazipeleka Yerusalemu.
8Namo mle Tibehati na Kuni iliyokuwa miji ya Hadarezeri Dawidi akachukua shaba nyekundu nyingi mno; ndizo, Salomo alizozitumia za kutengeneza ile bahari ya shaba nazo zile nguzo navyo vyombo vya shaba.[#1 Fal. 7:15,23.]
9Tou, mfalme wa Hamati, aliposikia, ya kuwa Dawidi amevipiga vikosi vyote vya Hadarezeri, mfalme wa Soba,
10akamtuma mwanawe Hadoramu kwake mfalme Dawidi kumpongeza na kumbariki, kwa kuwa amepigana na Hadarezeri na kumshinda, kwani Tou na Hadarezeri walikuwa wakipigana vita; akampelekea vyombo vyo vyote vya dhahabu na vya fedha na vya shaba.
11Hivi navyo mfalme Dawidi akavitakasa kuwa mali za Bwana kama fedha na dhahabu, alizoziteka kwa mataifa yote, kwa Waedomu na kwa Wamoabu na kwa wana wa Amoni na kwa Wafilisti na kwa Waamaleki.
12Naye Abisai, mwana wa Seruya, akawapiga Waedomu Bondeni kwa Chumvi, watu 18000.
13Kisha Dawidi akaweka askari kwa Waedomu, nao Waedomu wote wakawa watumishi wa Dawidi. Ndivyo, Bwana alivyompa Dawidi kushinda po pote, alipokwenda.
14Dawidi akawa mfalme wa Waisiraeli wote, akawatengenezea watu wake wote mashauri yaliyokuwa sawa, maana yaliongoka.
15Naye Yoabu, mwana wa Seruya, alikuwa mkuu wa vikosi, naye Yosafati, mwana wa Ahiludi, alikuwa mwandishi wa mambo yaliyopaswa kukumbukwa.
16Naye Sadoki, mwana wa Ahitubu, na Ahimeleki, mwana wa Abiatari, walikuwa watambikaji, naye Sausa alikuwa mwandishi.[#1 Mambo 24:6.]
17Naye Benaya, mwana wa Yoyada, alikuwa mkuu wa Wakreti na wa Wapuleti, nao wana wa Dawidi walikuwa wa kwanza mkononi kwa mfalme.