The chat will start when you send the first message.
1ILIYOBAKI, ndugu, tuombeeni, neno la Bwana liendelee, likatunzwe vilevile kama ilivyo kwenu;
2tukaokolewe na watu wasio haki, wahaya; maana si wote walio na imani.
3Lakini Bwana ni mwaminifu, atakaewafanyeni imara na kuwaokoeni na yule mwovu.
4Nasi tumemtumaini Bwana kwa mambo yenu, kwamba mnayafanya tuliyowaagizeni, tena kwamba mtayafanya.
5Bwana awaongozeni mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na uvumilivu wa Kristo.
6Twawaagizeni, ndugu, katika jina la Bwana wetu Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu na killa ndugu aendae bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.
7Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata, kwa sababu hatukwenda bila utaratibu kwenu;
8wala hatukula chakula kwa mtu ye yote burre, bali kwa taabu na masumbufu, mchana na usiku, tulitenda kazi, illi tusimlemee mtu kwenu;
9si kwamba hatuna uwezo, bali tufanye nafsi zetu kuwa mfano kwenu, mtufuate.
10Kwa maana hatta wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, bassi, asile chakula.
11Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawʼana shughuli yao wenyewe, bali wanajishughulisha na mambo ya wengine.
12Bassi twawaagiza, hao na kuwaonya katika Bwana wetu Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.
13Lakini, ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.
14Na ikiwa mtu aliye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizumgumze nae, apate kutahayarika;
15illakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
16Sasa, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani siku zote kwti njia zote. Bwana awe pamoja nanyi nyote.
17Salamu zangu mimi Paolo, kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndiyo alama katika killa waraka, ndivyo niandikavyo.
18Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amin.