The chat will start when you send the first message.
1BASSI ilipoamriwa tusafiri hatta Italia, wakamtia Paolo na wafungwa wengine katika mikono ya akida mmoja, jina lake Yulio, wa kikosi cha Augusto.
2Tukapanda katika merikebu ya Adramuttio iliyokuwa tayari kusafiri hatta miji ya pwani za Asia, tukatweka; Aristarko, Mmakedoni wa Thessalonika, akiwa pamoja nasi.
3Siku ya pili tukawasili Sidon; Yulio akamfadhili sana Paolo akampa rukhusa kwenda kwa rafiki zake, kutunzwa nao.
4Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kupro illi kuukinga upepo, kwa maana pepo zilikuwa za mbisho,
5tukaipita bahari ya upande wa Kilikia na Pamfulia, tukafikia Mura, mji wa Lukia.
6Na huko yule akida akakuta merikebu ya Iskanderia, tayari kusafiri hatta Italia, akatupandisha.
7Tukasafiri pole pole kwa muda wa siku nyingi, tukafika hatta Knido kwa shidda; na kwa sababu upepo ulikuwa ukituzuia tukapita chini ya Krete illi kuukinga upepo, tukaikabili Salmone.
8Tukaipita kwa shidda, pwani kwa pwani, tukafika mahali paitwapo Bandari Nzuri. Karibu na hapo pana mji uitwao Lasaya.
9Na wakati mwingi ulipokwisha kupita, na safari ikiwa ina khatari sasa kwa sababu siku za kufunga zilikuwa zimekwisha kupita, Paolo akawaonya, akawaambia,
10Wanaume, naoua kwamba safari hii itakuwa ina madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, illa na ya maisha zetu pia.
11Lakini yule akida akawasikiliza nakhodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paolo.
12Na kwa sababu bandari haikukaa vema, watu wakae ndani yake wakati wa haridi, walio wengi wakatoa shauri tutweke tukatoke huko illi wapate kufika Foiniki, kama ikiwezekana, na kukaa huko wakati wa baridi: nayo ni bandari ya Krete, inaelekea kaskazini-mashariki na kusini-mashariki.
13Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata walioazimu kupata, wakangʼoa nanga, wakasafiri karibu na Krete pwani kwa pwani.
14Baada ya muda mchache upepo wa nguvu wa namna ya tufani, uitwao Eurakulo, ukaipiga merikebu.
15Ikachukuliwa, maana haikuweza kushindana na upepo, tukaiacha tukiichukuliwa.
16Na tukipita upesi karibu na kisiwa kiitwacho Klaudia tukadiriki kuikweza mashua; kwa shidda lakini.
17Walipokwisha kuikweza wakatumia misaada, wakaikaza merikehu kwa kupitisha kamba chini yake; na wakiogopa wasije wakakwama kwenye Surtis, wakatua matanga wakachukuliwa vivi hivi.
18Na kwa kuwa tukawa tukipigwa sana na ile tufani, siku ya pili yake wakaanza kuitupa shehena baharini.
19Siku ya tatu tukatupa vyombo vya merikebu kwa mikono yetu wenyewe.
20Na jua na nyota hazikuonekana kwa muda wa siku nyingi, na tufani kuu ikatushika, bassi tukakata tamaa ya kuokoka.
21Na tulipokuwa tumekaa wakati mwingi bila kula chakula, Paolo akasimama katikati yao, akasema, Wanaume, ingalikuwa kheri kama mngalinisikiliza na kutokungʼoa nanga huko Krete, na kupata madhara haya na hasara hii.
22Sasa nawapeni shauri, mwe na moyo mkuu, kwa maana hapana hatta nafsi mmoja miongoni mwenu atakaepotea, illa merikebu, bassi.
23Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambae mimi ni mtu wake, na udiye nimtumikiae, alisimama karibu nami akaniambia,
24Usiogope, Paolo, huna buddi kusimama mbele ya Kaisari: tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
25Bassi, wanaume, changaʼmkani; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.
26Lakini hatuna buddi kupwelewa katika kisiwa kimoja.
27Hatta usiku wa kumi na nne ulipowadia, tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia inchi kavu.
28Wakatupa bildi wakakuta pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakakuta pima kumi na tano.
29Wakachelea wasije wakapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne, wakaomba kuche.
30Na baharia walipotaka kukimbia na kuiacha merikebu, wakiishusha mashua baharini kana kwamba wanataka kutupa nanga za omo,
31Paolo akawaambia akida na askari, Hawa wasipokaa ndani ya marikebu hamtaweza kuokoka.
32Bassi askari wakazikata kamba za mashua, wakaiacha ianguke.
33Na kulipokuwa kukipambazuka Paolo akawasihi wote wale chakula, akisema, Leo ni siku ya kumi na nne kungoja na kufunga, hamkula kitu cho chote.
34Bassi nawasihi mle chakula, maana itakuwa kwa wokofu wenu; kwa maana hapana unywele wa vichwa vyenu utakaopotea.
35Alipokwisha kusema haya akatwaa mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote akaumega akaanza kula.
36Wakachangaʼmka wote, wakala vyakula wenyewe.
37Na sisi tuliokuwa ndani ya merikebu tulipata watu miateen na sabaini na sita.
38Walipokwisha kushiba wakaipunguza shehena va merikebu, wakaitupa nganu baharini.
39Kulipokucha hawakuitambua ile inchi, illa waliona hori yenye ufuko, wakashauriana kuiegesha merikebu huko, kama ikiwezekana.
40Wakazitupilia mbali zile nanga, wakaziacha baharini, wakazilegeza kamba za sukani, wakalitweka tanga dogo illi liushike upepo, wakauendea ule ufuko.
41Lakini wakafikia mahali palipokutana bahari mbili, wakaiegesha merikebu, omo ikakwama ikakaa isitikiswe, bali shetri ilikuwa imefumuliwa kwa nguvu za mawimbi.
42Shauri la askari lilikuwa wafungwa wauawe, mtu asiogelee na kukimbia.
43Bali akida, akitaka kumponya Paolo, akawazuia, wasifanye kama walivyokusudia, akawaamuru wale wawezao kuogelea wajitupe baharini, wafike inchi kavu;
44nao waliosalia, hawa juu ya mbao na hawa juu ya vitu vingine vya merikebu. Na hivyo watu wote wakapata kuifikia inchi kavu salama.