Isaya 12

Isaya 12

Wimbo wa shukrani

1Siku hiyo mtasema:

“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,

maana ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imetulia,

nawe umenifariji.

2Mungu ndiye mwenye kuniokoa,[#12:2 Taz Kut 15:2; Zab 118:14]

nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;

Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;

yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”

3Mtachota maji kwa furaha

kutoka visima vya wokovu.

4Siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Mwenyezi-Mungu

mwombeni kwa jina lake.

Yajulisheni mataifa matendo yake,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa

kwa kuwa ametenda mambo makuu;

haya na yajulikane duniani kote.

6Pazeni sauti na kuimba kwa furaha,

enyi wakazi wa Siyoni,

maana aliye mkuu miongoni mwenu

ndiye Mungu, Mtakatifu wa Israeli.”

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania