Zaburi 120

Zaburi 120

Kuomba msaada

1Katika taabu yangu nilimwita Mwenyezi-Mungu,

naye akanijibu.

2Uniokoe ee Mwenyezi-Mungu,

na watu wadanganyifu na waongo.

3Enyi watu wadanganyifu, mtapewa kitu gani?

Mtaadhibiwa namna gani?

4Kwa mishale mikali ya askari,

kwa makaa ya moto mkali!

5Ole wangu kwamba naishi kama mgeni huko Mesheki;

naishi kama mgeni katika mahema ya Kedari.

6Nimeishi muda mrefu mno

kati ya watu wanaochukia amani!

7Wakati ninaposema nataka amani,

wao wanataka tu vita.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania