Zaburi 128

Zaburi 128

Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu

1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,

wanaoishi kufuatana na amri zake.

2Utapata matunda ya jasho lako,

utafurahi na kupata fanaka.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;

watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.

4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.

5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!

Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.

6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!

Amani iwe na Israeli!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania