Zaburi 134

Zaburi 134

Msifuni Mungu

1Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote,

enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake.

2Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu,

na kumtukuza Mwenyezi-Mungu!

3Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni;

yeye aliyeumba mbingu na dunia.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania