1 Wamakabayo 12

1 Wamakabayo 12

Ushirika na Roma na Sparta

1Yonathani alipoona mambo yanamwendea vizuri, akachagua wajumbe na kuwatuma Roma kwenda kufufua na kuthibitisha urafiki na Waroma.

2Aidha alipeleka barua zenye ujumbe kama huo Sparta na mahali pengine.

3Hao wajumbe wakaenda Roma, ambako walikaribishwa katika Baraza Kuu la Wazee. Wakasema: “Yonathani, kuhani mkuu, na taifa la Wayahudi wametutuma kuja kufufua urafiki na ushirikiano ule wa awali na Roma.”

4Waroma wakawapa barua za utambulisho kwa wakuu wa kila nchi ambayo wajumbe hao wangepita wakati wa kurudi Yudea, wakiomba wapatiwe usalama.

5Ifuatayo ni nakala ya barua ambayo Yonathani aliwaandikia Wasparta:

19“Ifuatayo ni nakala ya barua yenu ya awali kwa Onia:

Kampeni za Yonathani na Simoni

24Ndipo Yonathani akapata habari kwamba maofisa wa Demetrio walikuwa wamekuja tena, na jeshi kubwa zaidi, kumshambulia yeye.

25Yonathani hakutaka kuwapa fursa ya kuivamia nchi yake. Kwa hiyo akaondoka Yerusalemu, akaenda kupambana nao katika eneo la Hamathi.

26Akapeleka wapelelezi kambini kwa maadui, wakarudi na kumwarifu ya kwamba maadui walikuwa wanafanya mipango kuwashambulia Wayahudi usiku.

27Hivi, jua lilipotua, Yonathani akawaamuru askari wake wote kukaa chonjo, silaha mkononi, tayari kwa shambulio lolote la ghafla saa za usiku. Pia aliwaweka askari walinzi kuzunguka kambi yote.

28Maadui waliposikia kwamba Yonathani na watu wake walikuwa wamejitayarisha kwa mapambano, wakaingiwa na hofu kubwa, wakakimbia na kuacha mioto inawaka kambini.

29Yonathani na watu wake waliona hiyo mioto ya kambini, lakini hawakutambua yaliyokuwa yametukia mpaka kesho yake asubuhi.

30Ndipo Yonathani akaondoka kuwafuata maadui. Lakini hakuweza kuwakuta kwa sababu walikuwa wamekwisha vuka mto Eleuthero.

31Basi, Yonathani akageuka, akashika njia ya pembeni na kuwashambulia Wazabadea, kabila moja la Waarabu. Aliwashinda, akateka mali yao.

32Halafu akaondoka hapo na kwenda Damasko, akipita kulikagua eneo lote la huko.

33Simoni naye aliondoka akapitia katika nchi ile akafika mbele hadi Askaloni na ngome za jirani. Halafu akageuka na kwenda Yopa, akautwaa mji huo kwa ghafla,

34maana alikuwa amesikia kwamba wenyeji wake walikuwa tayari kuwakabidhi ngome ya Yopa askari waliokuwa wametumwa na Demetrio. Simoni akaweka kikosi cha askari kuilinda ngome hiyo.

35Yonathani aliporejea, aliitisha mkutano wa wazee wa watu kufanya mipango ya kujenga maboma katika Yudea,

36kuongeza urefu wa kuta za Yerusalemu, na kujenga ukuta mrefu kati ya ngome na mji, ili kuitenga hiyo ngome, maadui washindwe kununua au kuuza chochote.

37Watu wakafanya kazi pamoja kuimarisha ukuta wa mji, kwa sababu sehemu ya ukuta wa upande wa mashariki ilikuwa imeanguka; aliitengeneza pia sehemu iliyoitwa Kafenatha.

38Simoni naye akaujenga upya mji wa Adida katika tambarare ya Shefela, akauimarisha na kuuwekea milango na mapingo.

Trifo amteka Yonathani

39Baada ya hayo, Trifo akafanya mbinu za kumpindua mfalme Antioko ili awe yeye mfalme wa Asia.

40Hata hivyo, aliogopa kwamba Yonathani asingekubaliana naye kuhusu mpango huo, na angeanzisha vita dhidi yake kuzuia jambo hilo. Hivi, Trifo akawa anatafuta kumkamata na kumuua; hivyo akaondoka, akaenda Beth-sheani.

41Lakini, Yonathani akaenda kumkabili huko Beth-sheani na askari waliochaguliwa 40,000.

42Trifo alipoona ukubwa wa jeshi la Yonathani, akaogopa kuanza uchokozi.

43Hivi, akampokea Yonathani kwa heshima zote, akamtambulisha kwa washauri wake wote, akampa zawadi, na kuwaagiza washauri wake na askari wake wamtii Yonathani kama walivyokuwa wanamtii yeye mwenyewe.

44Halafu akamwuliza Yonathani: “Kwa nini umewataabisha kiasi kikubwa hivyo hawa askari wako wakati ambapo hatupigani vita?

45Kwa nini usiwarudishe nyumbani? Chagua watu wachache wabaki nawe, na halafu unisindikize huko Tolemai. Nitakupatia mji huo wa Tolemai, pamoja na ngome nyinginezo, na askari, na maofisa wao wote. Halafu mimi nitakwenda zangu nyumbani. Hiyo ndiyo iliyonileta hapa.”

46Yonathani akaamini maneno hayo. Basi, kufuatana na hayo aliyosema Trifo, akawarudisha askari wake Yudea.

47Alijiwekea watu 3,000; 2,000 akawaacha Galilaya, na 1,000 tu wakafuatana naye.

48Lakini mara Yonathani alipoingia Tolemai, wakazi wake wakafunga milango ya mji, wakamkamata yeye na kuwaua wote aliokuwa amefuatana nao.

49Kisha Trifo akapeleka vikosi vya askari wa miguu na wapandafarasi Galilaya na kwenye Bonde la Yezreeli kwenda kuwaua askari wa Yonathani waliobaki.

50Hao askari Wayahudi wakahisi kwamba Yonathani alikuwa amekamatwa na kuuawa pamoja na wale waliokuwa wamefuatana naye. Hivi wakatiana moyo, wakajipanga kwa vita.

51Majeshi ya adui yaliposogea na kuona Wayahudi wamejipanga tayari kutetea maisha yao, wakarudi nyuma.

52Ndipo askari Wayahudi wakarejea Yudea salama, lakini wenye hofu. Taifa zima likaangua kilio kikubwa, kumlilia na kumwombolezea Yonathani na wenzake.

53Nayo mataifa yote ya jirani sasa yalijaribu kuwaangamiza Wayahudi. Walidhani kwamba Wayahudi hawakuwa na kiongozi tena wala msaidizi. Wakasema: “Ngoja tuwapige sasa na kufutilia mbali kumbukumbu yao duniani.”

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania