The chat will start when you send the first message.
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Heri mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,
anayefurahia sana kutii amri zake.
2Wazawa wake watakuwa wenye nguvu nchini;
watoto wa wanyofu watapata baraka.
3Nyumbani kwake kutakuwa na mali nyingi;
uadilifu wake wadumu milele.
4Mtu mwema huangaziwa mwanga gizani;
mtu mwenye huruma, mpole na mwadilifu.
5Mtu mkarimu akopeshaye bila faida, hufanikiwa;
mtu afanyaye shughuli zake kwa kutumia haki.
6Mwadilifu hatashindwa kamwe,
huyo atakumbukwa milele.
7Hana haja ya kuogopa akipata habari mbaya;[#112:6-7 Haisemwi kwamba wenye kumtii Mungu hawatapata shida; watazipata lakini hazitawashinda kwa sababu tegemeo lao liko kwa Mungu (taz pia 37:39-40 maelezo).]
ana moyo thabiti na humtegemea Mwenyezi-Mungu.
8Yuko imara moyoni, wala hataogopa;
naye atawaona maadui zake wanashindwa.
9Hutoa kwa ukarimu, huwapa maskini;
uadilifu wake wadumu milele.
Nguvu yake inatukuzwa kwa heshima.
10Watu waovu huona hayo na kuudhika;
husaga meno kwa chuki na kutoweka,
matazamio ya mtu mbaya huishia patupu.