The chat will start when you send the first message.
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Enyi watumishi wa Mwenyezi-Mungu, lisifuni jina lake!
2Jina lake litukuzwe,
sasa na hata milele.
3Kutoka mashariki na hata magharibi,[#113:3 Manaeno yanayotumika kusema ulimwenguni kote (50:1; Mal 1:11).]
litukuzwe jina la Mwenyezi-Mungu!
4Mwenyezi-Mungu atawala juu ya mataifa yote,
utukufu wake wafika juu ya mbingu.
5Nani aliye kama Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu?
Yeye ameketi juu kabisa;
6lakini anatazama chini,
azione mbingu na dunia.
7Humwinua fukara kutoka mavumbini;[#113:7 neno linalotumiwa kimfano na linamaanisha hali duni ya kukandamizwa. Taz msemo wa namna hiyo hiyo katika 1Sam 2:4-8; Luka 1:46-53.]
humnyanyua maskini kutoka unyonge wake,
8na kumweka pamoja na wakuu;
pamoja na wakuu wa watu wake.
9Humjalia mwanamke tasa furaha nyumbani kwake;
humfurahisha kwa kumjalia watoto.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!