Isaya 12

Isaya 12

Kushukuru na kusifu

1Katika siku ile utasema:

“Nitakusifu wewe, Ee Bwana .

Ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imegeukia mbali

nawe umenifariji.

2Hakika Mungu ni wokovu wangu;

nitamtumaini wala sitaogopa.

Bwana , Bwana , ni nguvu zangu na wimbo wangu;

amekuwa wokovu wangu.”

3Kwa furaha mtachota maji

kutoka visima vya wokovu.

4Katika siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Bwana , mliitie jina lake;

julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5Mwimbieni Bwana , kwa kuwa ametenda mambo makuu,

hili na lijulikane duniani kote.

6Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,

kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.