Ayubu 26

Ayubu 26

Ayubu anajibu: Utukufu wa Mungu hauchunguziki

1Kisha Ayubu akajibu:

2“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo!

Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!

3Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima?

Nayo ni busara gani kubwa uliyoonesha!

4Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo?

Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?

5“Wafu wako katika maumivu makuu,

wale walio chini ya maji,

na wale wanaoishi ndani yake.

6Mauti iko wazi mbele za Mungu;[#26:6 yaani Kuzimu ; Kiebrania ni Sheol]

Uharibifu haukufunikwa.

7Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu;

naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.

8Huyafungia maji kwenye mawingu yake,

hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.

9Huufunika uso wa mwezi mpevu,

akitandaza mawingu juu yake.

10Amechora mstari wa upeo juu ya maji,

ameweka mpaka wa nuru na giza.

11Nguzo za mbingu nazo zatetemeka,

zinatishika anapozikemea.

12Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari;

kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.

13Aliisafisha anga kwa pumzi yake;

kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.

14Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake;

tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu!

Ni nani basi awezaye kuelewa

ngurumo za nguvu zake?”

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.