Zaburi 54

Zaburi 54

Zaburi 54

Kuomba ulinzi wa Mungu kutokana na adui

1Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,

unifanyie hukumu kwa uwezo wako.

2Ee Mungu, sikia maombi yangu,

usikilize maneno ya kinywa changu.

3Wageni wananishambulia,

watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,

watu wasiomjali Mungu.

4Hakika Mungu ni msaada wangu,

Bwana ndiye anayenitegemeza.

5Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,

kwa uaminifu wako uwaangamize.

6Nitakutolea dhabihu za hiari;

Ee Bwana , nitalisifu jina lako

kwa kuwa ni vyema.

7Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,

na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.