The chat will start when you send the first message.
1*Kulikuwa na mtu wa Mafariseo, jina lake Nikodemo, aliyekuwa mkuu wa Wayuda.[#Yoh. 7:50; 19:39.]
2Huyo akamjia na usiku, akamwambia: Mfunzi mkuu, tunajua, ya kuwa wewe u mfunzi aliyetoka kwa Mungu, kwani hakuna mtu anayeweza kuvifanya vielekezo hivyo, unavyovifanya wewe, Mungu asipokuwa naye.
3Yesu akajibu, akamwambia: Kweli kweli nakuambia: Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.[#1 Petr. 1:23.]
4Nikodemo akamwambia: Mtu atawezaje kuzaliwa akiisha kuwa mzee? Ataweza kuingia tena tumboni mwa mama yake, apate kuzaliwa?
5Yesu akajibu: Kweli kweli nakuambia: Mtu asipozaliwa majini na Rohoni, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu;[#Ez. 36:25-27; Mat. 3:11; Ef. 5:26; Tit. 3:5.]
6kilichozaliwa na mwili ni mwili, nacho kilichozaliwa na Roho ni roho.[#Yoh. 1:13; 1 Mose 5:3; Sh. 51:7; Rom. 8:5-9.]
7Usistaajabu, nikikuambia: Sharti mzaliwe mara ya pili!
8Upepo huvuma, upendako, nawe huusikia uvumi wake, lakini hujui, uanziako wala ukomeako. Hivyo ndivyo, kila aliyezaliwa Rohoni alivyo.
9Nikodemo alipojibu na kumwuliza: Haya yawezekanaje kuwapo?
10Yesu akajibu, akamwambia: Je? Wewe u mfunzi wa Isiraeli, tena haya huyatambui?
11Kweli kweli nakuambia: Sisi huyasema, tuyajuayo; huyashuhudia, tuliyoyaona, lakini hamwupokei ushuhuda wetu![#Yoh. 7:16; 8:26,28.]
12Msiponitegemea, nikiwaambia mambo ya ulimwenguni, mtanitegemeaje, nikiwaambia mambo ya mbinguni?
13Tena hakuna aliyepaa mbinguni, asipokuwa Mwana wa mtu aliyeshuka toka mbinguni.[#Ef. 4:9.]
14Kama Mose alivyokweza nyoka jangwani, vivyo hivyo hata Mwana wa mtu sharti akwezwe,[#4 Mose 21:8-9.]
15kila amtegemeaye apate uzima wa kale na kale.*
16*Kwani kwa hivyo, Mungu alivyoupenda ulimwengu, alimtoa Mwana wake wa pekee, kila amtegemeaye asiangamie, ila apate uzima wa kale na kale.[#Rom. 5:8; 8:32; 1 Yoh. 4:9.]
17Kwani Mungu hakumtuma Mwana wake ulimwenguni, auhukumu ulimwengu, ila ulimwengu upate kuokolewa naye.[#Yoh. 12:47.]
18Amtegemeaye hahukumiwi; asiyemtegemea amekwisha kuhukumiwa, kwani hakulitegemea Jina la Mwana wa Pekee wa Mungu[#Yoh. 3:36; 5:24.]
19Nayo hukumu ndiyo hii: mwanga ulikuja ulimwenguni, lakini watu waliipenda giza kuliko mwanga, kwa sababu matendo yao yalikuwa mabaya,[#Yoh. 1:5,9-11.]
20kwani kila mwenye kutenda maovu huuchukia mwanga, haji mwangani, matendo yake yasipatilizwe;[#Ef. 5:13.]
21lakini mwenye kuyafanya yaliyo ya kweli huja mwangani, matendo yake yaonekane, ya kuwa yametendeka katika Mungu.*
22Kisha Yesu na wanafunzi wake wakaenda katika nchi ya Yudea, akashinda kule pamoja nao akibatiza.[#Yoh. 4:1-2.]
23Lakini Yohana alikuwa akibatizia Enoni karibu ya Salemu, kwani kule kulikuwa na maji mengi, tena ndiko, watu walikomwendea, wakabatizwa naye,
24maana Yohana alikuwa hajatiwa bado kifungoni.[#Mat. 14:3.]
25Ikawa, wanafunzi wa Yohana walipobishana na Myuda kwa sababu ya maosho,
26wakaja kwa Yohana, wakamwambia: Mfunzi mkuu, aliyekuwa pamoja na wewe kule ng'ambo ya Yordani, yule uliyemshuhudia wewe, tazama, huyo anabatiza, watu wote wakimwendea.[#Yoh. 1:26-34; 4:1-2.]
27Yohana akajibu, akasema: Hakuna, mtu awezacho kukitwaa, asichopewa toka mbinguni.[#Ebr. 5:4.]
28Ninyi wenyewe mwanishuhudia, ya kuwa nalisema: Mimi siye Kristo ila nimetumwa, nimtangulie yeye.[#Yoh. 1:20,23,27.]
29Aliye mwenye mchumba ndiye bwana arusi; lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama na kumsikiliza hufurahi sana kwa kuisikia sauti yake bwana arusi; basi, hiyo furaha yangu imetimia.[#Mat. 9:15; 22:2.]
30Yeye sharti akue, nami sharti nipunguke.
31Anayekuja toka juu ni mkuu kuliko wote; aliyetoka chini ni wa nchini, husema yaliyo ya nchini; anayekuja toka mbinguni ni mkuu kuliko wote.[#Yoh. 8:23.]
32Aliyoyaona nayo aliyoyasikia, ndiyo, anayoyashuhudia, lakini hakuna anayeupokea ushuhuda wake.[#Yoh. 3:11.]
33Aupokeaye ushuhuda wake huyu anamtambulisha Mungu waziwazi, kuwa ni wa kweli;[#1 Yoh. 5:10.]
34kwani aliyetumwa na Mungu huyasema maneno yake Mungu, naye Mungu haigawii Roho kwa kuipima.[#Yoh. 1:33-34.]
35Baba humpenda Mwana, akampa yote mkononi mwake.[#Yoh. 5:20; Mat. 11:27.]
36Amtegemeaye Mwana anao uzima wa kale na kale, lakini asiyemtii Mwana hataona uzima, ila makali ya Mungu humkalia.[#Yoh. 3:18.]