The chat will start when you send the first message.
1Kama Bwana asingalikuwa nasi, Waisiraeli na waseme hivyo:
2Kama Bwana asingalikuwa nasi, watu walipotuinukia,
3wangalitumeza, tukingali wazima bado; ilikuwa hapo, moto wa makali yao ulipotuunguza.
4Maji mengi yangalitudidimiza hapo, mito ilipopita juu yetu,[#Sh. 42:8; 69:16.]
5kwani hapo mafuriko ya maji yaliyopita juu yetu yangalitutosa kweli.
6Bwana na asifiwe! Kwani hakututoa, tunyafuliwe na meno yao!
7Roho zetu zimepona, kama ndege anavyopona tanzini, kamba za tanzi zikikatika; ndivyo, sisi tulivyopona nasi.
8Msaada wetu uko katika Jina la Bwana, ndiye aliyeziumba mbingu na nchi.[#Sh. 121:2.]