Mashangilio 26

Mashangilio 26

Kujiombea wokovu.

1Kwa kuwa mimi nimeendelea pasipo kosa, niamulie, Bwana! Bwana ndiye, nimwegemeaye pasipo kutikisika.

2Nijaribu, Bwana, na kunipima, unichuje mafigo, hata moyo![#Sh. 17:3.]

3Kwani wema wako uko machoni pangu, nami huendelea kukuwia mwelekevu.

4Sikai pamoja na watu walio wapuzi tu, wala walio wenye kinyume siingii mwao.[#Sh. 1:1.]

5Ninachukizwa na mkutano wao wafanyao mabaya, wala sikai pamoja nao wambezao Mungu.

6Nitainawa mikono yangu kwa maji yaondoayo makosa, kisha nitatokea kuzunguka mezani pako, Bwana;[#Sh. 122.]

7ndipo, nitakapozipaza sauti, nikushukuru nikiyasimulia makuu yako yote ya kustaajabu.

8Bwana, napapenda hapo, Nyumba yako ilipo, ndipo mahali, unapokaa utukufu wako.[#Sh. 27:4.]

9Usiikusanye roho yangu pamoja nazo zao wakosaji! Usininyime uzima pamoja nao wauao wenzao!

10Mikononi mwao yamo mapotovu, mikono yao ya kuume imejaa mapenyezo.

11Lakini mimi ninaendelea pasipo kosa; kwa kunihurumia nikomboe!

12Miguu yangu huenda paliponyoka, nimtukuze Bwana katika mikutano.[#Sh. 22:23.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania