The chat will start when you send the first message.
1Kila apendaye mafundisho hupenda maarifa;
Bali yeye achukiaye kulaumiwa ni kama mnyama.
2Mtu mwema atapata upendeleo kwa BWANA;
Bali mtu wa hila atahukumiwa naye.
3Mtu hatathibitika kwa njia ya uovu;
Shina la mwenye haki halitaondolewa kamwe.
4Mwanamke mwema ni taji la mumewe;[#Mit 31:23; 1 Kor 11:7; Mit 14:30]
Bali aaibishaye ni kama kuoza mifupani mwake.
5Mawazo ya mwenye haki ni adili;
Bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa.
6Maneno ya waovu huotea damu;
Bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa.
7Waovu huangamia, hata hawako tena;[#Mt 7:24]
Bali nyumba ya mwenye haki itasimama.
8Mtu atasifiwa kwa kadiri ya akili zake;[#1 Sam 13:13; Mal 2:8,9; Mit 1:25,26; 3:35; Mt 27:4,5]
Bali mwenye moyo wa ukaidi atadharauliwa.
9Afadhali mtu anayedharauliwa, ikiwa ana mtumwa,
Kuliko ajisifuye, ikiwa anahitaji chakula.
10Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake;[#Kum 25:4]
Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
11Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele;[#Mwa 3:19; Mit 28:19; Efe 4:28; 1 The 4:11]
Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.
12Asiye haki hutamani nyavu za wabaya;[#Zab 1:3; Lk 8:15]
Bali shina lao wenye haki huleta matunda.
13Katika kosa la midomo kuna mtego kwa mbaya;[#2 Pet 2:9]
Bali mwenye haki atatoka katika taabu.
14Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake;[#Isa 3:10]
Na atarudishiwa matendo ya mikono yake.
15Njia ya mpumbavu imenyoka machoni pake mwenyewe;[#Lk 18:11]
Bali yeye aliye na hekima husikiliza shauri.
16Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara;
Bali mtu mwerevu husitiri aibu.
17Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki;
Bali shahidi wa uongo hutamka hila.
18Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga;
Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.
19Mdomo wa kweli utathibitishwa milele;[#Zek 1:5,6]
Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.
20Hila imo mioyoni mwao wafikirio uovu;
Bali wafanyao mashauri ya amani, kwao kuna furaha.
21Mwenye haki hatapatikana na msiba wowote;[#Rum 8:28; 2 The 1:6; 2 Pet 2:9]
Bali wasio haki watajazwa mabaya.
22Midomo ya uongo ni chukizo kwa BWANA;[#Ufu 22:15]
Bali watendao uaminifu ndio furaha yake.
23Mwanadamu mwenye busara husitiri maarifa;
Bali moyo wa wapumbavu hutangaza upumbavu.
24Mkono wa mwenye bidii utatawala;[#1 Fal 11:28; Mit 10:4]
Bali mvivu atalipishwa kodi.
25Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha;[#Isa 50:4]
Bali neno jema huufurahisha.
26Mwenye haki ni kiongozi wa mwenzake;
Bali njia ya wasio haki huwakosesha.
27Mtu mvivu hapiki mawindo yake;
Bali mwenye bidii anazo mali za thamani.
28Katika njia ya haki kuna uhai;[#Kum 30:15; Mt 19:17; Rum 5:21; 2 Kor 4:17; Ufu 2:7]
Wala hakuna mauti katika mapito yake.