The chat will start when you send the first message.
1Mbona nyakati zisiwekwe na Mwenyezi?[#Mdo 1:7]
Na hao wamjuao mbona hawazioni siku zake?
2Wako waziondoao alama za mipaka;[#Kum 19:14]
Huyachukua makundi kwa jeuri na kuyalisha.
3Humfukuza punda wake asiye baba,[#Kum 24:6,10,12,17]
Humtwaa rehani ng’ombe wake mwanamke mjane.
4Humgeuza mhitaji aiache njia;[#Mit 28:28]
Maskini wa nchi hujificha pamoja.
5Tazama, kama punda-mwitu jangwani
Wao hutoka kwenda kazini mwao, wakitafuta chakula kwa bidii;
Jangwa huwapa chakula cha watoto wao.
6Hukata nafaka zao mashambani;
Na kuokota zabibu za waovu.
7Hujilaza usiku kucha uchi pasipo nguo,[#Kut 22:26; Kum 24:12; Isa 58:7]
Wala hawana cha kujifunika baridi.
8Hutota kwa manyunyo ya milimani,[#Omb 4:5]
Na kuambatana na jabali kwa kukosa sitara,
9Wako wamwondoao matitini kwa nguvu huyo asiye na baba,
Na kutwaa rehani kwa maskini;
10Hata wazunguke uchi pasipo mavazi,
Nao wakiwa na njaa huchukua miganda;
11Hushindika mafuta ndani ya makuta ya watu hao;
Wakanyaga mashinikizo, nao wana kiu.
12Watu huugua toka mji ulio na watu wengi,[#Mhu 8:11]
Na roho yake aliyejeruhiwa hupiga ukelele;
Wala Mungu hauangalii upumbavu.
13Hawa ni katika hao waliouasi mwanga;
Hawazijui njia zake,
Wala hawakai katika mapito yake.
14Mwuaji huamka asubuhi kukipambauka, huwaua maskini na wahitaji;
Tena wakati wa usiku yu kama mwivi.
15Tena jicho lake mzinifu hungojea wakati wa giza-giza,
Akisema, Hapana jicho litakaloniona;
Naye huuficha uso wake.
16Wao hutoboa nyumba gizani;[#Yn 3:20]
Hujifungia ndani wakati wa mchana;
Hawaujui mwanga.
17Kwani asubuhi kwao wote ni kama giza tupu;
Kwani wao wavijua vitisho vya hiyo giza tupu.
18Mwasema, Yeye ni mwepesi juu ya uso wa gharika;
Sehemu yao inalaaniwa duniani;
Hageuki kwenda njia ya mizabibuni.
19Chaka na hari hukausha maji ya theluji;
Kuzimu nako hao ambao wamefanya dhambi.
20Tumbo lililomzaa litamsahau; buu litamla na kuona tamu;[#Mit 10:7]
Hatakumbukwa tena;
Na udhalimu utavunjwa kama mti.
21Naam, yeye huwala walio tasa wasiozaa;
Wala hamtendei mema mwanamke mjane.
22Lakini Mungu huwadumisha wenye uwezo kwa nguvu zake;
Huinuka, wasiokuwa na tumaini la kuishi.
23Huwapa kuwa na salama, nao wapumzika kwayo;
Na macho yake ya juu ya njia zao.
24Wao wametukuzwa; lakini kitambo kidogo hutoweka;[#Zab 37:35,36]
Naam, hushushwa, na kuondolewa njiani kama wengine wote,
Nao hukatwa kama vile masuke ya ngano.
25Na kama sivyo sasa, ni nani atakayenihukumu kuwa ni mwongo,
Na kuyafanya maneno yangu kuwa si kitu?