Zab 100

Zab 100

Nchi zote Zaitwa Kumsifu Mungu

1Mfanyieni BWANA shangwe, dunia yote;

2Mtumikieni BWANA kwa furaha;

Njoni mbele zake kwa kuimba;

3Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;[#Ayu 10:8,9; Mhu 12:1; Efe 2:10; Eze 34:30]

Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;

Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.

4Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru;

Nyuani mwake kwa kusifu;

Mshukuruni, lihimidini jina lake;

5Kwa kuwa BWANA ndiye mwema;[#1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 106:1; 107:1; 118:1; 136:1; Yer 33:11]

Rehema zake ni za milele;

Na uaminifu wake vizazi na vizazi.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania