Zab 111

Zab 111

Sifa kwa Maajabu ya Mungu

1Haleluya.[#111:1 maana yake ni, Msifuni BWANA.]

Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote,

Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.

2Matendo ya BWANA ni makuu,[#Ayu 38:1]

Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.

3Kazi yake ni heshima na adhama,

Na haki yake yakaa milele.

4Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;

BWANA ni mwenye fadhili na rehema.

5Amewapa wamchao chakula;

Atalikumbuka agano lake milele.

6Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,

Kwa kuwapa urithi wa mataifa.

7Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,[#Zab 19:7]

Maagizo yake yote ni amini,

8Yamethibitika milele na milele,[#Ufu 15:3]

Yamefanywa katika kweli na adili.

9Amewapelekea watu wake ukombozi,

Ameamuru agano lake liwe la milele,

Jina lake ni takatifu la kuogopwa.

10Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,[#Kum 4:6; Ayu 28:28; Mit 1:7; 9:10; Mhu 12:3]

Wote wafanyao hayo wana akili njema,

Sifa zake zakaa milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania