Zab 126

Zab 126

Mavuno ya Shangwe

1BWANA alipowarejeza mateka wa Sayuni,[#Mdo 12:9]

Tulikuwa kama waotao ndoto.

2Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko,[#Ayu 8:21]

Na ulimi wetu kelele za furaha.

Ndipo waliposema katika mataifa,

BWANA amewatendea mambo makuu.

3BWANA alitutendea mambo makuu,

Tulikuwa tukifurahi.

4Ee BWANA, uwarejeze watu wetu waliofungwa,

Kama vijito vya Kusini.

5Wapandao kwa machozi[#Isa 12:1-3; Yer 31:9; Yoe 2:17; Mt 5:4; 2 Kor 7:8-11]

Watavuna kwa kelele za furaha.

6Ingawa mtu anakwenda zake akilia,

Azichukuapo mbegu za kupanda.

Hakika atarudi kwa kelele za furaha,

Aichukuapo miganda yake.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania