Zab 13

Zab 13

Sala ya Ukombozi kutoka kwa Adui

1Ee BWANA, hata lini utanisahau, hata milele?[#Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2]

Hata lini utanificha uso wako?

2Hata lini nifanye mashauri nafsini mwangu,

Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?

Hata lini adui yangu atukuke juu yangu?

3Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;[#Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14]

Uyatie nuru macho yangu,

Nisije nikalala usingizi wa mauti.

4Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;

Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.

5Nami nimezitumainia fadhili zako;[#2 Nya 20:12]

Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.

6Naam, nimwimbie BWANA,

Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania