Zab 14

Zab 14

Kushutumiwa kwa Wasiomwamini Mungu

1Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;[#Rum 3:10-12; Zab 10:4; Mit 1:7,22; Mwa 6:12]

Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,

Hakuna atendaye mema.

2Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,

Aone kama yuko mtu mwenye akili,

Amtafutaye Mungu.

3Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,

Hakuna atendaye mema,

La! Hata mmoja.

4Je! Wote wafanyao maovu hawajui?

Walao watu wangu kama walavyo mkate,

Hawamwiti BWANA.

5Hapo ndipo walipoingiwa na hofu nyingi,

Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.

6Mnalitia aibu shauri la mtu mnyonge,

Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.

7Laiti wokovu wa Israeli utoke katika Sayuni!

BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;

Yakobo atashangilia,

Israeli atafurahi.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania