Zab 23

Zab 23

Mchungaji Mwema

1BWANA ndiye mchungaji wangu,[#Yn 10:11; 1 Pet 2:25]

Sitapungukiwa na kitu.

2Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,[#Ufu 7:17; Eze 34:14]

Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza

Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,[#Zab 46:11; Isa 8:10; Zek 8:23; Mt 1:23; Mdo 18:9,10]

Sitaogopa mabaya;

Kwa maana Wewe upo pamoja nami,

Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.

5Waandaa meza mbele yangu,

Machoni pa watesi wangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

Na kikombe changu kinafurika.

6Hakika wema na fadhili zitanifuata[#2 Kor 5:1]

Siku zote za maisha yangu;

Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania