Zab 48

Zab 48

Utukufu wa Nguvu za Sayuni

1Bwana ndiye aliye mkuu,[#Isa 2:2; Oba 1:17; Mik 4:1]

Na mwenye kusifiwa sana.

Katika mji wa Mungu wetu,

Katika mlima wake mtakatifu.

2Kuinuka kwake ni mzuri sana,[#Mt 5:35; Yer 3:19; Omb 2:15; Eze 20:6; Isa 14:13]

Ni furaha ya dunia yote.

Mlima Sayuni pande za kaskazini,

Mji wa Mfalme mkuu.

3Mungu katika majumba yake

Amejijulisha kuwa ngome.

4Maana, tazama, wafalme walikusanyika;[#2 Sam 10:6]

Walipita wote pamoja.

5Waliona, mara wakashangaa;

Wakafadhaika na kukimbia.

6Papo hapo tetemeko liliwashika,

Utungu kama wa mwanamke azaaye.

7Kwa upepo wa mashariki[#Eze 27:26]

Wavunja jahazi za Tarshishi.

8Kama tulivyosikia, ndivyo tulivyoona,[#Isa 2:2; Mik 4:1]

Katika mji wa BWANA wa majeshi.

Mji wa Mungu wetu;

Mungu ataufanya imara hata milele.

9Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu,

Katikati ya hekalu lako.

10Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu,[#Mal 1:11]

Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia.

Mkono wako wa kuume umejaa haki;

11Na ufurahi mlima Sayuni.

Binti za Yuda na washangilie

Kwa sababu ya hukumu zako.

12Tembeeni katika Sayuni,

Uzungukeni mji,

Ihesabuni minara yake,

13Tieni moyoni boma zake,

Yafikirini majumba yake,

Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.

14Kwa maana ndivyo alivyo[#Isa 25:9]

MUNGU, Mungu wetu.

Milele na milele

Yeye ndiye atakayetuongoza.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania