Zaburi 114

Zaburi 114

Mungu na watu wake

1Watu wa Israeli walipotoka Misri,

wazawa wa Yakobo walipotoka ugenini,

2Yuda ikawa maskani ya Mungu,

Israeli ikawa milki yake.

3Bahari iliona hayo ikakimbia;

mto Yordani ukaacha kutiririka!

4Milima ilirukaruka kama kondoo dume;

vilima vikaruka kama wanakondoo!

5Ee bahari, imekuwaje hata ukakimbia?

Nawe Yordani, kwa nini ukaacha kutiririka?

6Enyi milima, mbona mliruka kama kondoo dume?

Nanyi vilima, mmerukaje kama wanakondoo?

7Tetemeka, ee dunia mbele yake Mwenyezi-Mungu;

tetemeka mbele ya Mungu wa Yakobo,

8anayeugusa mwamba ukawa bwawa la maji,

nayo majabali yakawa chemchemi za maji!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania