Zaburi 70

Zaburi 70

Kuomba msaada

1Upende kuniokoa ee Mungu!

Ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.

2Wanaonuia kuniangamiza,

na waaibike na kufedheheka!

Hao wanaotamani niumie,

na warudi nyuma na kuaibika.

3Hao wanaonisimanga,

na wapumbazike kwa kushindwa kwao.

4Lakini wote wale wanaokutafuta,

wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.

Wapendao wokovu wako,

waseme daima: “Mungu ni mkuu!”

5Nami niliye maskini na fukara,

unijie haraka, ee Mungu!

Ndiwe msaada wangu na mkombozi wangu;

ee Mwenyezi-Mungu, usikawie!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania