Zaburi 128

Zaburi 128

Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu

1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,

wanaoishi kufuatana na amri zake.

2Utapata matunda ya jasho lako,

utafurahi na kupata fanaka.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;

watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.

4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.

5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!

Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.

6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!

Amani iwe na Israeli!

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  
Published by: Bible Society of Tanzania