Mashangilio 2

Mashangilio 2

Machafuko ya watu yatavunjwa na Masiya.Sh. 37:18Iy. 23:102 Tim. 2:19

1Mbona wamizimu hupiga makelele? Mbona makabila ya watu huwaza mambo yaliyo ya bure?[#Tume. 4:25-30.]

2Wafalme wa nchi hushikana mioyo, wakuu nao hula njama wakikaa pamoja, wamkatae Bwana na Masiya wake kwamba:[#Ufu. 11:18; 19:19.]

3Na tuyavunje mafungo yao! na tuzitupe kamba zao, zisitufunge tena![#Yer. 2:20; 5:5; Luk. 19:14.]

4Lakini akaaye mbinguni anawacheka, yeye Bwana anawafyoza.[#Sh. 37:13; 59:9.]

5Siku zitakapotimia, atasema nao kwa makali yake, awastushe kwa moto wa machafuko yake:[#Yes. 34; Ufu. 6:15-17.]

6Mimi nimemsimika mfalme wangu huko mlimani kwa Sioni kwenye utukufu wangu.

7Nitasimulia shauri, Bwana aliloniambia: Wewe ndiwe Mwanangu, siku hii ya leo mimi nimekuzaa.[#2 Sam. 7:14; Sh. 89:27-30; Tume. 13:33; Ebr. 1:5; 5:5.]

8Omba kwangu! Nami nitakupa wamizimu, wawe fungu lako, nayo mapeo ya nchi, yawe mali zako![#Dan. 7:13-14; Ebr. 1:2.]

9Kwa fimbo ya chuma utawaponda, kama vyombo vya mfinyanzi utawavunja.[#Ufu. 2:27; 12:5; 19:15.]

10Sasa nyie wafalme, pambanukeni! Nanyi waamuzi wa nchi, onyekani!

11Mtumikieni Bwana kwa kumwogopa! Mshangilieni kwa kutetemeka![#Fil. 2:12; Ebr. 12:28.]

12Mnoneeni Mwana, asiwatolee makali, mkaangamia njiani! Maana moto wa makali yake utawaka upesi. Wenye shangwe ndio wote wamwegemeao![#1 Sam. 10:1; Sh. 34:9; 84:13; Yes. 30:18; Yoh. 3:36.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania