Zaburi 12

Zaburi 12

Ombi la msaada wakati wa dhiki

1Tuokoe, ee BWANA, maana hamna tena amchaye Mungu[#Isa 57:1]

Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.

2Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,

Wenye midomo ya kujipendekeza;

Husemezana kwa mioyo ya unafiki;

3BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,

Na ulimi unenao maneno ya kiburi;

4Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;

Midomo yetu ni yetu wenyewe,

Ni nani aliye bwana juu yetu?

5Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,[#Kut 3:7,8]

Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,

Sasa nitasimama, asema BWANA,

Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.

6Maneno ya BWANA ni maneno safi,[#2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5]

Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi;

Iliyosafishwa mara saba.

7Wewe, BWANA, ndiwe utakayetuhifadhi,

Utatulinda na kizazi hiki milele.

8Wasio haki hutembea pande zote,

Huku ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya