The chat will start when you send the first message.
1BWANA, ni nani atakayekaa[#Zab 2:5]
Katika hema yako?
Ni nani atakayeishi
Katika kilima chako kitakatifu?
2Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,[#Zab 84:11; Isa 33:15,16]
Na kutenda haki.
Asemaye kweli kwa moyo wake,
3Asiyesingizia kwa ulimi wake.
Wala kumtenda mwenziwe mabaya,
Wala kumsengenya jirani yake.
4Anayedharau waovu Machoni pake,[#Yos 9:18-20]
Bali huwaheshimu wamchao BWANA
Aliyeapa ingawa kwa hasara yake,
Hayabadili maneno yake.
5Asiyetoa fedha yake apate kula riba,[#Eze 18:8,9]
Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia.
Mtu atendaye mambo hayo
Hataondoshwa milele.