Zaburi 100

Zaburi 100

Wimbo wa sifa

1Mshangilieni Mwenyezi-Mungu, enyi nchi zote!

2Mwabuduni Mwenyezi-Mungu kwa furaha,

nendeni kwake mkiimba kwa shangwe!

3Jueni kwamba Mwenyezi-Mungu ni Mungu.

Yeye ndiye aliyetuumba, nasi ni mali yake;

sisi ni watu wake, ni kondoo wa malisho yake.

4Pitieni milango ya hekalu lake kwa shukrani,

ingieni katika nyua zake kwa sifa.

Mshukuruni na kulisifu jina lake.

5Mwenyezi-Mungu ni mwema;[#Taz Zab 106:1; 107:1; 136:1]

fadhili zake zadumu milele,

na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania