The chat will start when you send the first message.
1Utenzi wangu kuhusu uaminifu na haki;
ninauimba kwa heshima yako, ee Mwenyezi-Mungu.
2Nitazingatia mwenendo usio na hatia.
Je, utakuja kwangu lini?
Nitaishi kwa unyofu nyumbani kwangu;
3sitavumilia kamwe upuuzi.
Nayachukia matendo ya watu wapotovu,
mambo yao hayataambatana nami.
4Upotovu wowote ule uwe mbali nami;
sitahusika kabisa na uovu.
5Anayemsengenya jirani nitamfutilia mbali;
sitamvumilia mwenye majivuno na kiburi.
6Nitawaangalia kwa wema watu walio waaminifu,
wapate kuishi pamoja nami.
Watu wanyofu ndio watakaonitumikia.
7Mwongo yeyote hatakaa nyumbani mwangu;
hakuna msema uongo atakayekaa kwangu.
8Siku kwa siku nitawaangamiza waovu wote nchini;
nitawaangamiza wabaya wote mjini mwa Mwenyezi-Mungu.