Zaburi 11

Zaburi 11

Kumtumainia Mungu

1Kwake Mwenyezi-Mungu nakimbilia usalama;

mnawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege, mpaka milimani,

2maana waovu wanavuta pinde;

wameweka mishale tayari juu ya uta,

wawapige mshale watu wema gizani!

3Kama misingi ikiharibiwa,

mtu mwadilifu atafanya nini?”

4Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;

kiti cha enzi cha Mwenyezi-Mungu kiko mbinguni.

Kwa macho yake huwachungulia wanadamu,

na kujua kila kitu wanachofanya.

5Mwenyezi-Mungu huwapima waadilifu na waovu;

huwachukia kabisa watu wakatili.

6Atawanyeshea waovu makaa ya moto na madini ya kiberiti;

upepo wa hari utakuwa ndio adhabu yao.

7Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu na apenda uadilifu;

watu wanyofu watakaa pamoja naye.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania