Zaburi 110

Zaburi 110

Kutawazwa kwa mfalme mteule

1Mwenyezi-Mungu amwambia bwana wangu:[#Taz Mat 22:44; Marko 12:36; Luka 20:42:43; Mate 2:34-35; 1Kor 15:25;]

“Keti upande wangu wa kulia,

hata niwaweke maadui zako chini ya miguu yako.”

2Mwenyezi-Mungu ataeneza enzi yako kutoka Siyoni;

utatawala juu ya maadui zako wote.

3Watu wako watakujia kwa hiari,

siku utakapokwenda kuwapiga maadui.

Juu ya milima mitakatifu watakujia vijana wako,

kama umande unaotokeza alfajiri mapema.

4Mwenyezi-Mungu amekuapia wala hatabadili nia yake:[#Taz Ebr 5:6; 6:20; 7:17,21]

“Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”

5Bwana yuko upande wako wa kulia;

atawaponda wafalme atakapokasirika.

6Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi;

atawaponda viongozi kila mahali duniani.

7Mfalme atakunywa maji ya kijito njiani;

naye atainua kichwa juu kwa ushindi.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania