Zaburi 126

Zaburi 126

Kuomba nguvu mpya

1Mwenyezi-Mungu alipoturekebisha na kuturudisha Siyoni,

tulikuwa kama watu wanaoota ndoto!

2Hapo tuliangua kicheko;

tulishangilia kwa furaha.

Nao watu wa mataifa mengine walisema:

“Mwenyezi-Mungu amewatendea mambo makubwa!”

3Kweli Mwenyezi-Mungu alitutendea mambo makubwa,

tulifurahi kwelikweli!

4Ee Mwenyezi-Mungu, urekebishe tena hali yetu,

kama mvua inavyotiririsha maji katika mabonde makavu.

5Wanaopanda kwa machozi,

watavuna kwa shangwe.

6Wanaokwenda kupanda mbegu wakilia,

watarudi kwa furaha wakichukua mavuno.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania