Zaburi 54

Zaburi 54

Sala ya kujikinga na maadui

1Uniokoe, ee Mungu, kwa jina lako;

unitetee kwa nguvu yako.

2Uisikie, ee Mungu, sala yangu;

uyategee sikio maneno ya kinywa changu.

3Watu wenye kiburi wananishambulia;

wakatili wanayawinda maisha yangu,

watu ambao hawamjali Mungu.

4Najua Mungu ni msaada wangu,

Mwenyezi-Mungu hutegemeza maisha yangu.

5Yeye atawaadhibu maadui zangu kwa uovu wao wenyewe;

kwa uaminifu wako, ee Mungu, uwaangamize.

6Nitakutolea tambiko kwa moyo mkunjufu;

nitakushukuru kwa kuwa ni vema.

7Maana umeniokoa katika taabu zangu zote,

nami nimewaona maadui zangu wameshindwa.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania