Zaburi 4

Zaburi 4

Kuomba msaada jioni

1Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.

Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;

unionee huruma na kusikia sala yangu.

2Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?

Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?

3Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.

Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.

4Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;

tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.

5Toeni tambiko zilizo sawa,[#4:5 Yaani matoleo au tambiko zisizochanganyika na dhambi (Isa 1:10-17) au zenye kutokana na upendo na kumjua Mungu kikweli (Hos 6:6; Amo 5:21-25).]

na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.

6Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!

Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”

7Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,

kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.

8Nalala na kupata usingizi kwa amani;

ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania