Zaburi 122

Zaburi 122

Zaburi 122

Sifa kwa Yerusalemu

1Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,

“Twende nyumbani mwa Mwenyezi Mungu.”

2Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama

malangoni mwako.

3Yerusalemu imejengwa vyema kama mji

ulioshikamana pamoja.

4Huko ndiko makabila hukwea,

makabila ya Mwenyezi Mungu,

kulisifu jina la Mwenyezi Mungu kulingana na maagizo

waliopewa Israeli.

5Huko viti vya hukumu hukaa,

viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.

6Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:

“Wote wanaokupenda na wawe salama.

7Amani na iwe ndani ya kuta zako,

na usalama ndani ya ngome zako.”

8Kwa ajili ya ndugu na rafiki zangu,

nitasema, “Amani iwe ndani yako.”

9Kwa ajili ya nyumba ya Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,

nitatafuta mafanikio yako.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.