Zaburi 125

Zaburi 125

Zaburi 125

Usalama wa watu wa Mwenyezi Mungu

1Wale wamtumainio Mwenyezi Mungu ni kama Mlima Sayuni,

ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.

2Kama milima inavyozunguka Yerusalemu,

ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowazunguka watu wake

sasa na hata milele.

3Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi

waliyopewa wenye haki,

ili wenye haki wasije wakatumia

mikono yao kutenda ubaya.

4Ee Mwenyezi Mungu, watendee mema walio wema,

wale walio wanyofu wa moyo.

5Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka,

Mwenyezi Mungu atawafukuza pamoja na watenda maovu.

Amani iwe juu ya Israeli.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.