Zaburi 4

Zaburi 4

Zaburi 4

Sala ya jioni ya kuomba msaada

1Nijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Nipumzishe katika shida zangu;

nirehemu, usikie ombi langu.

2Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu hadi lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo hadi lini?

3Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwana atanisikia nimwitapo.

4Katika hasira yako, usitende dhambi.

Tulieni kimya mkiwa vitandani mwenu,

mkiichunguza mioyo yenu.

5Toeni dhabihu zilizo haki;

mtegemeeni Bwana .

6Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonesha jema lolote?”

Ee Bwana , tuangazie nuru ya uso wako.

7Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

8Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana ,

waniwezesha kukaa kwa salama.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.